Mkalamo yavutia, kwa kadhaa vivutio
Vichache takutajia, litege lako sikio
Kwanza mji umekua, wamepita wapitao
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Vichache takutajia, litege lako sikio
Kwanza mji umekua, wamepita wapitao
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Mandari za kubarizi, kusepa hutotamani
Kama mto MSANGAZI, kigong’ondo Ufingoni
Japo kwenye kiangazi, maji hakuna mtoni
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Maji yaliyotuwaa, mabwawa maji baridi
Kama vile muangaa, Kwembosha kwa musabedi
Watu hunywa na kufua, kunywesha hawana budi
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Imepita kati reli, usafirishaji mwema
Kwa treni na toroli, Tanga to Darisalama
Huzisafirisha mali, salmini na salama
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Mashamba ya kupendeza, ya miembe na minazi
Muhunguru hadi boza, tizama neema hizi
Macho yako huliwaza, uendapo matembezi
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Umeme ni wera wera, mataa kila sehemu
Sehemu za biashara, zinapendeza kaumu
Mtihani bara bara, ndo kidogo nalaumu
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Mitaa yake minono, kwa tamu zake lahaja
Tongani hadi chamwino, sisahau Mtakuja
Sokoni hasa ndo mno, kwa bwana Mitumba ROJA
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Kuna kabila kadhaa, zilizopo kwenye chati
Wazigua ndio taa, ndo wenyeji wenye hati
Wagogo na wasambaa, sasa wapo wamang’ati
Kijiji kinavutia, ukifika utapenda
Viko vingi vidokezo, viwanja vya kujidai
Kwenye game na michezo, ni mtini na kindii
Watu huonesha uwezo, BUSHI dafu hawafui
Kijiji kinavutia, ukifika utapenda
Usafiri abiria, wa kudumu si mapito
Mkata ukitokea, utakuja na KIDATO
Pangani kielekea, utauvuka na mto
Kijiji kinavutia, ukifika utapenda
Karibu wangu JIRANI, nyumbani karibu sana
Ndugu zangu wa Sadani, Kwamsisi nawaona
Karibu wa Mikocheni, Mkwaja mpaka Bweni
Karibuni karibuni, sisi watu wakarimu
Ya mwisho kadi tamati, yanatosha nilosema
Naivaa yangu shati, hapa ndo mwisho nakoma
Pongezi zangu za dhati, kwako wewe ulo soma
Siku iwe njema kwako, iache yako coment.
Kama mto MSANGAZI, kigong’ondo Ufingoni
Japo kwenye kiangazi, maji hakuna mtoni
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Maji yaliyotuwaa, mabwawa maji baridi
Kama vile muangaa, Kwembosha kwa musabedi
Watu hunywa na kufua, kunywesha hawana budi
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Imepita kati reli, usafirishaji mwema
Kwa treni na toroli, Tanga to Darisalama
Huzisafirisha mali, salmini na salama
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Mashamba ya kupendeza, ya miembe na minazi
Muhunguru hadi boza, tizama neema hizi
Macho yako huliwaza, uendapo matembezi
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Umeme ni wera wera, mataa kila sehemu
Sehemu za biashara, zinapendeza kaumu
Mtihani bara bara, ndo kidogo nalaumu
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Mitaa yake minono, kwa tamu zake lahaja
Tongani hadi chamwino, sisahau Mtakuja
Sokoni hasa ndo mno, kwa bwana Mitumba ROJA
Naipenda Mkalamo, Mungu ameibariki
Kuna kabila kadhaa, zilizopo kwenye chati
Wazigua ndio taa, ndo wenyeji wenye hati
Wagogo na wasambaa, sasa wapo wamang’ati
Kijiji kinavutia, ukifika utapenda
Viko vingi vidokezo, viwanja vya kujidai
Kwenye game na michezo, ni mtini na kindii
Watu huonesha uwezo, BUSHI dafu hawafui
Kijiji kinavutia, ukifika utapenda
Usafiri abiria, wa kudumu si mapito
Mkata ukitokea, utakuja na KIDATO
Pangani kielekea, utauvuka na mto
Kijiji kinavutia, ukifika utapenda
Karibu wangu JIRANI, nyumbani karibu sana
Ndugu zangu wa Sadani, Kwamsisi nawaona
Karibu wa Mikocheni, Mkwaja mpaka Bweni
Karibuni karibuni, sisi watu wakarimu
Naivaa yangu shati, hapa ndo mwisho nakoma
Pongezi zangu za dhati, kwako wewe ulo soma
Siku iwe njema kwako, iache yako coment.
COMMENTS