SURA YA KWANZA UKODISHAJI WA SHAMBA Baada ya kupata wazo la kulima, tulianza kuulizia mahala ambapo tunaweza kupata shamba kwa ajili ...
SURA YA
KWANZA
UKODISHAJI
WA SHAMBA
Baada ya kupata wazo la kulima, tulianza kuulizia mahala ambapo tunaweza
kupata shamba kwa ajili ya kukodisha. Maeneo ambayo tunafanya kazi (UHINDINI –
MBEYA) kulikuwa na jirani yetu ambae alikuwa anafanya kazi ya ulinzi katika
Bank ya Equity, ambaye alijulikana kwa jina la Shega. Kwa kuwa huyu alikuwa ni
mwenyeji wa huku tuliona ni bora kufanya mawasiliano nae afanye michakato.
Baada ya muda alitupa majibu kuwa alipata shamba maeneno fulani katika
Wilaya ya Mbozi Mkoa huu wa Mbeya. Hivyo alizungumza na jamaa zake wa huko.
Jambo lilipokuwa tayari tuliamua kwenda na kuliona hilo shamba na kufanya
makubaliano. Tulipanga siku rasmi ya kwenda huko.
Siku ya jumapili tarehe 15/10/2017 ndio siku ambayo tuliamua kwenda huko
shambani. tulianza safari majira ya saa 4 za asubuhi tukiwa watu wane ambao ni
bwana Ummari (Baba la baba), Afande Shega, Ben Oiso pamoja na Mimi (Saidi
Bunduki). Kiongozi wa safari hii alikuwa ni bwana Ummar (Baba la baba). Sehemnu
ambayo tulikuwa tunakwenda ni kijiji kiitwacho Senjele. Kijiji ambacho
kinapatikana takriban kilomita 45 kutoka Mbeya mjini kuelekea TUNDUMA.
Safari hii ilikuwa ni kwajili ya kwenda kuliona shamba ambalo tumekusudia
kukodisha kwa ajili ya kilimo cha mahindi. Tulifika Senjele majira ya saa 6 mchana na kumsubiri mwenyeji
wetu ambaye ndiye aliyekuwa amefanya michakato ya kutafuta hilo shamba. Jamaa
yule anaitwa SIMON alikuwa anatokea Songwe. Huyu ndiye alikuwa na mawasiliano
na bwana Shega. Baada ya muda kidogo alikuja na kutukuta tumekaa chini ya
muembe mdogo uliopo pale njiani kijijini.
Lakini pia kuja kwake bado haikuwa mafanikio kwa sababu, huyo bwana
ambaye ndiye mwenye shamba alikuwa hayupo, hivo bado kulikuwa na haja ya
kumsubiri na kufanyanaye maelewano kuhusu shamba. Pia muda ule tuliutumia kwa
ajili ya kwenda kuliona hilo shamba ambalo lilikuwa linasemekana kuwa lilikuwa
na ukubwa wa ekari sita. Kwa bahati nzuri shamba halikuwa mbali na bara bara
kuu ya Tunduma.
Pia tulifurahi kuona shamba likiwa katika hali nzuri sana. Hii ni kwa
sababu msimu uliopita lililimwa na baada ya hapo pia lilisafishwa kwa ajili ya
kujiandaa na kilimo cha mwaka huu. Kwahiyo halikuwa na miti wala majani. Labda
tu lilikuwa na haja ya kuchimbua tena na ng’ombe kwa ajili ya kuboresha zaidi.
Na pia kwa kuwa tulikuwa tumechelewa kutafuta mashamba, haikuwa rahisi kwa muda
ule kupata shamba kwa urahisi na hata kama tungepata isingekuwa rahisi kupata
shamba lililo karibu na makazi ya watu au barabara kama vile.
Mpaka muda huu tulikuwa watu watano, kwa sababu tayari alikuwa
ameshaongezeka jamaa mmoja (Simon). Huyu jamaa anaishi katika Kijiji
kinachoitwa NANYALA. Nanyala ni kijiji kilicho nyuma kidogo ya kile kijiji cha
Senjele. Hivi ni vijiji ambavyo vina mchanganyiko wa makabila ya Wanyakyusa na
Wanyiha. Na haya miongoni mwa makabila makubwa Mkoani Mbeya.
Picha halisi ikionesha
shamba jinsi lilivokuwa siku ya kwanza ambayo tulifika SENJELE. (Picha na Omy
Krish)
Upande mwingine wa
shamba. Kwa mbali zinaonekana nyumba za kijiji cha Senjele (Picha na Omy Krish)
Tulilikagua vema na kuridhika nalo kwa wakati huo tukimsubiri bwana
NICKSON ambaye ndiye mwenye eneo lile. Lakini baada ya kufanya mawasiliano naye
iligundulika kuwa alikuwa mbali kidogo na pale hivo aliomba kama kuna uwezekano
tufanye maelewano na mke wake. Tulifanya hivyo lakini mwishowe mke wake
alishindwa kufanya makubaliano kwa sababu
alikuwa na hofu juu ya kupunguza bei. Kwa hiyo ilitulazimu kumsubiri bwana
Nick.
Mpaka muda ule tayari ilikuwa ni saa nane za
mchana na njaa zilianza kututafuna. Hivyo ilibidi tuangalie sehemu ya kupata
chakula. Kwakweli sehemu ya kupata chakula kidogo ilikuwa ni changamoto kwa
sababu Senjele ni kijijini sana hivyo hapakuwa na migahawa ya kutosha. Lakini baadaye jamaa ambaye ndiye
alikuwa mwenyeji wetu ambaye ni SIMON alitupeleka sehemu ya pili ya mji ule
ambapo tulifanikiwakupata huduma ya chakula. Tulifanikiwa kupata wali
maharage pamoja na nyama za kuchoma za mbuzi.
COMMENTS